14 - (ق) عَنْ أَبِي ذَرٍّ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صلّى الله عليه وسلّم: (أَتَانِي آتٍ مِنْ رَبِّي، فَأَخْبَرَنِي ـ أَوْ قَالَ: بَشَّرَنِي ـ أَنَّهُ مَنْ مَاتَ مِنْ أُمَّتِي لاَ يُشْرِكُ بِاللهِ شَيْئاً، دَخَلَ الجَنَّةَ) . قُلْتُ: وَإِنْ زَنَى وَإِنْ سَرَقَ؟ قَالَ: (وَإِنْ زَنَى وَإِنْ سَرَقَ) .
Kutoka kwa Abuu Dhari -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Nilikuwa pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika ardhi yenye mawe katika mji wa Madina, tukaelekea mlima Uhudi, akasema: "Ewe Abuu Dhari" nikasema: Labbaika (nimekuitikia) Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu. Akasema: "Hainifurahishi mimi kumiliki dhahabu mfano wa mlima huu wa Uhudi, zikapita siku tatu nikawa hata na dinari moja (katika mali hiyo) isipokuwa kiasi ninachokihifadhi kwaajili ya kulipa deni, isipokuwa niseme kwa waja wa Mwenyezi Mungu hivi na vile." akigeuka kuliani kwake na kushotoni kwake, na nyuma yake, kisha akatembea, Akasema: "Hakika wenye vingi ndio wenye vichache siku ya kiyama isipokuwa atakayezungumza kwa mali hivi na vile hivi na vile" akageuka kuliani kwake na kushotoni kwake na nyuma yake, "Na wachache katika wao" kisha akasema kuniambia "Bakia hapo usitoke mpaka nikujie" kisha akaondoka katika giza la usiku mpaka akapotelea, nikasikia sauti imenyanyuka, nikapata hofu isijekuwa kuna mtu kamvamia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- nikataka kumfuata nikakumbuka kauli yake "Bakia hapo usitoke mpaka nikujie" nikabakia mpaka aliponijia, nikasema: Nilisikia sauti nikaingiwa na hofu sana, nikamuelezea akasema: "Hivi uliisikia?" Nikasema: Ndiyo, akasema: "Huyo ni Jibril alinijia akasema: Atakayekufa katika umma wako hamshirikishi Mwenyezi Mungu na kitu chochote ataingia peponi" Nikasema: Hata akizini na akaiba? Akasema: "Hata akizini na akaiba".
قال تعالى: {يَاأَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلاَ تَمُوتُنَّ إِلاَّ وَأَنْتُمْ مُسْلِمُونَ *}. [آل عمران:102]
[خ1237/ م94]