Books of Jame` al-Osool al-Tis`ah min al-Sunnah al-Mutahharh, Ma`alim al-Sunnah al-Nabawiyyah, and al-Wajeez fi al-Sunnah al-Nabawiyyah

The Sunnah of the Prophet.. Accessible to Everyone

image descriptions

Jame` al-Osool al-Tis`ah min al-Sunnah al-Mutahharh

45 Books
image descriptions

Ma`alim al-Sunnah al-Nabawiyyah

51 Books
image descriptions

al-Wajeez fi al-Sunnah al-Nabawiyyah

43 Books
image descriptions

al Ahadith al Kulliyyah

20 Books

Most Viewed

View all

قال تعالى: {وَمَا أُمِرُوا إِلاَّ لِيَعْبُدُوا اللَّهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ}. [البينة:5]

4 - (ق) عن عُمَرَ بْنِ الخَطَّابِ رضي الله عنه قَالَ: سَمِعْتُ النَّبِيَّ صلّى الله عليه وسلّم يَقُولُ: (يَا أَيُّهَا النَّاسُ! إِنَّمَا الْأَعْمَالُ بِالنِّيَّةِ [1] ، وَإِنَّمَا لاِمْرِئٍ مَا نَوَى، فَمَنْ كَانَتْ هِجْرَتُهُ إِلَى اللهِ وَرَسُولِهِ [2] ، فَهِجْرَتُهُ إِلَى اللهِ وَرَسُولِهِ، وَمَنْ هَاجَرَ إِلَى دُنْيَا يُصِيبُهَا، أَوْ امْرَأَةٍ يَتَزَوَّجُهَا، فَهِجْرَتُهُ إِلَى مَا هَاجَرَ إِلَيْهِ) .

Kutoka kwa Omari bin Khattwabi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika matendo yote huzingatiwa nia, na hakika kila mtu hulipwa kwa lile alilolinuia, atakayekuwa kuhama kwake ni kwaajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake basi (malipo yake yatakuwa) ni kwaajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na atakayekuwa kuhama kwake ni kwaajili ya dunia au ataipata au kwaajili ya mwanamke ili amuoe, basi kuhama kwake kutakuwa ni kwa lile alilolihamia".

10 - (م) عَن ابْنِ شُمَاسَةَ المَهْرِيِّ قَالَ: حَضَرْنَا عَمْرَو بْنَ العَاصِ وَهُوَ فِي سِيَاقَةِ المَوْتِ [1] ، فَبَكَى طَوِيلاً وَحَوَّلَ وَجْهَهُ إِلَى الجِدَارِ، فَجَعَلَ ابْنُهُ يَقُولُ: يَا أَبَتَاهُ! أَمَا بَشَّرَكَ رَسُولُ اللهِ صلّى الله عليه وسلّم بِكَذَا؟ أَمَا بَشَّرَكَ رَسُولُ اللهِ صلّى الله عليه وسلّم بِكَذَا؟ قَالَ: فَأَقْبَلَ بِوَجْهِهِ، فَقَالَ: إِنَّ أَفْضَلَ مَا نُعِدُّ شَهَادَةُ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللهُ وَأَنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ اللهِ، إِنِّي قَدْ كُنْتُ عَلَى أَطْبَاقٍ ثَلاَثٍ [2] :
لَقَدْ رَأَيْتُنِي وَمَا أَحَدٌ أَشَدَّ بُغْضاً لِرَسُولِ اللهِ صلّى الله عليه وسلّم مِنِّي، وَلاَ أَحَبَّ إِلَيَّ أَنْ أَكُونَ قَدْ اسْتَمْكَنْتُ مِنْهُ فَقَتَلْتُهُ، فَلَوْ مُتُّ عَلَى تِلْكَ الحَالِ لَكُنْتُ مِنْ أَهْلِ النَّارِ.
فَلَمَّا جَعَلَ اللهُ الْإِسْلاَمَ فِي قَلْبِي، أَتَيْتُ النَّبِيَّ صلّى الله عليه وسلّم، فَقُلْتُ: ابْسُطْ يَمِينَكَ فَلْأُبَايِعْكَ، فَبَسَطَ يَمِينَهُ، قَالَ: فَقَبَضْتُ يَدِي. قَالَ: (مَا لَكَ يَا عَمْرُو) ؟ قَالَ قُلْتُ: أَرَدْتُ أَنْ أَشْتَرِطَ قَالَ: (تَشْتَرِطُ بِمَاذَا) ؟ قُلْتُ: أَنْ يُغْفَرَ لِي، قَالَ: (أَمَا عَلِمْتَ أَنَّ الْإِسْلاَمَ يَهْدِمُ مَا كَانَ قَبْلَهُ؟ وَأَنَّ الهِجْرَةَ تَهْدِمُ مَا كَانَ قَبْلِهَا؟ وَأَنَّ الحَجَّ يَهْدِمُ مَا كَانَ قَبْلَهُ) ؟.
وَمَا كَانَ أَحَدٌ أَحَبَّ إِلَيَّ مِنْ رَسُولِ اللهِ صلّى الله عليه وسلّم، وَلاَ أَجَلَّ فِي عَيْنِي مِنْهُ، وَمَا كُنْتُ أُطِيقُ أَنْ أَمْلَأَ عَيْنَيَّ مِنْهُ إِجْلاَلاً لَهُ، وَلَوْ سُئِلْتُ أَنْ أَصِفَهُ مَا أَطَقْتُ، لِأَنِّي لَمْ أَكُنْ أَمْلَأُ عَيْنَيَّ مِنْهُ، وَلَوْ مُتُّ عَلَى تِلْكَ الحَالِ لَرَجَوْتُ أَنْ أَكُونَ مِنْ أَهْلِ الجَنَّةِ.
ثُمَّ وَلِينَا أَشْيَاءَ مَا أَدْرِي مَا حَالِي فِيهَا، فَإِذَا أَنَا مُتُّ، فَلاَ تَصْحَبْنِي نَائِحَةٌ وَلاَ نَارٌ، فَإِذَا دَفَنْتُمُونِي؛ فَشُنُّوا عَلَيَّ التُّرَابَ
[3]
شَنّاً، ثُمَّ أَقِيمُوا حَوْلَ قَبْرِي قَدْرَ مَا تُنْحَرُ جَزُورٌ، وَيُقْسَمُ لَحْمُهَا، حَتَّى أَسْتَأْنِسَ بِكُمْ، وَأَنْظُرَ مَاذَا أُرَاجِعُ بِهِ رُسُلَ رَبِّي.

Kutoka kwa bin Shammasa Al Mihriy Amesema:Tulifika kwa Amru bin Aaswi naye akiwa katika safari ya kifo, akalia kwa muda mrefu, na akageuza uso wake kuelekea ukutani, mwanaye akaanza kusema, Ewe baba yangu, kwani hakukubashiria Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake kwa jambo kadhaa (yaani pepo)? kwani hakukubashiria Mtume-Rehema na Amani ziwe juu yake kwa jambo kadhaa? akageuka kwa uso wake, kisha akasema: Hakika jambo bora katika yale tunayoyaandaa ni kushuhudia kuwa Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Hakika mimi nilikuwa katika hali za aina tatu: Nilijikuta mimi kuwa hakuna anayemchukia kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuliko mimi, Na hakuna kitu nilichotamani zaidi kama kumtia mikononi ili nimuue, basi lau ningekufa katika hali hiyo ningekuwa ni katika watu wa motoni, Basi Mwenyezi Mungu alipouweka Uislamu moyoni mwangu, nilimuendea Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- Kisha nikasema: Nyoosha mkono wako wa kulia ili nikupe utiifu wangu kwako, basi akanyoosha mkono wake wa kulia nikakunja mkono wangu, akasema: "Umekuwaje wewe Amru?" Nikasema: Nilitaka niweke sharti kwanza, akasema: "Unaweka sharti la kitu gani?" Nikasema: Nisamehewe, akasema: "Hivi hukujua kuwa uislamu hufuta makosa yaliyokuwa kabla yake, na kuwa kuhama kunafuta makosa yaliyokuwa kabla yake, nakuwa Hija hufuta makosa yaliyokuwa kabla yake?" Kuanzia hapo hapakuwa tena na yeyote niliyempenda zaidi kuliko Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- wala niliyemuheshimu zaidi machoni mwangu kuliko yeye, Na sikuwa naweza kumtazama kwa macho yangu; kwasababu ya kumuheshimu, na hata kama ningeombwa nimsifie nisingeweza; kwasababu mimi sikuwa naweza kumtazama kwa macho yangu, na lau ningekufa katika hali hiyo ningetaraji kuwa miongoni mwa watu wa peponi, Kisha tukatawala mambo ambayo mpaka sasa sijui hali yangu ndani yake? Basi ikiwa nitakufa nisifuatwe na maombolezo wala moto, na mkinizika, basi nimwagieni udongo kidogo kidogo, kisha bakini kaburini kwangu kwa kiasi cha muda wa kuweza kumchinja ngamia na kumchuna, na kugawanywa nyama yake, ili nijiliwaze kwenu, na nisubiri nini nitawajibu wajumbe wa Mola wangu.

14 - (ق) عَنْ أَبِي ذَرٍّ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صلّى الله عليه وسلّم: (أَتَانِي آتٍ مِنْ رَبِّي، فَأَخْبَرَنِي ـ أَوْ قَالَ: بَشَّرَنِي ـ أَنَّهُ مَنْ مَاتَ مِنْ أُمَّتِي لاَ يُشْرِكُ بِاللهِ شَيْئاً، دَخَلَ الجَنَّةَ) . قُلْتُ: وَإِنْ زَنَى وَإِنْ سَرَقَ؟ قَالَ: (وَإِنْ زَنَى وَإِنْ سَرَقَ) .

Kutoka kwa Abuu Dhari -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Nilikuwa pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika ardhi yenye mawe katika mji wa Madina, tukaelekea mlima Uhudi, akasema: "Ewe Abuu Dhari" nikasema: Labbaika (nimekuitikia) Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu. Akasema: "Hainifurahishi mimi kumiliki dhahabu mfano wa mlima huu wa Uhudi, zikapita siku tatu nikawa hata na dinari moja (katika mali hiyo) isipokuwa kiasi ninachokihifadhi kwaajili ya kulipa deni, isipokuwa niseme kwa waja wa Mwenyezi Mungu hivi na vile." akigeuka kuliani kwake na kushotoni kwake, na nyuma yake, kisha akatembea, Akasema: "Hakika wenye vingi ndio wenye vichache siku ya kiyama isipokuwa atakayezungumza kwa mali hivi na vile hivi na vile" akageuka kuliani kwake na kushotoni kwake na nyuma yake, "Na wachache katika wao" kisha akasema kuniambia "Bakia hapo usitoke mpaka nikujie" kisha akaondoka katika giza la usiku mpaka akapotelea, nikasikia sauti imenyanyuka, nikapata hofu isijekuwa kuna mtu kamvamia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- nikataka kumfuata nikakumbuka kauli yake "Bakia hapo usitoke mpaka nikujie" nikabakia mpaka aliponijia, nikasema: Nilisikia sauti nikaingiwa na hofu sana, nikamuelezea akasema: "Hivi uliisikia?" Nikasema: Ndiyo, akasema: "Huyo ni Jibril alinijia akasema: Atakayekufa katika umma wako hamshirikishi Mwenyezi Mungu na kitu chochote ataingia peponi" Nikasema: Hata akizini na akaiba? Akasema: "Hata akizini na akaiba".

15 - (ق) عن أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ: أَنَّ النَّبِيَّ صلّى الله عليه وسلّم ـ وَمُعاذٌ رَدِيفُهُ عَلَى الرَّحْلِ ـ قَالَ: (يَا مُعَاذُ بْنَ جَبَلٍ) ! قَالَ: لَبَّيْكَ يَا رَسُولَ اللهِ وَسَعْدَيْكَ [1] ! قَالَ: (يَا مُعَاذُ) ! قَالَ: لَبَّيْكَ يَا رَسُولَ اللهِ وَسَعْدَيْكَ! ثَلاَثاً، قَالَ: (مَا مِنْ أَحَدٍ يَشْهَدُ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللهُ وَأَنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ اللهِ، صِدْقاً مِنْ قَلْبِهِ؛ إِلاَّ حَرَّمَهُ اللهُ عَلَى النَّارِ) . قَالَ: يَا رَسُولَ اللهِ! أَفَلاَ أُخْبِرُ بِهِ النَّاسَ فَيَسْتَبْشِرُوا؟ قَالَ: (إِذاً يَتَّكِلُوا) . وَأَخْبَرَ بِهَا مُعَاذٌ عِنْدَ مَوْتِهِ تَأَثُّماً [2] .

Kutoka kwa Anas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Yakwamba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- na Mua'dh akiwa nyuma yake juu ya kipandwa, Alisema: "Ewe Mua'dh" Akasema: Labaika Wasa'daika- Nimekuitikia kwa furaha yako- Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Alisema: "Ewe Mua'dh" Akasema: Labaika Wasa'daika- Nimekuitikia kwa furaha yako- Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Alisema: "Ewe Mua'dh" Akasema: Labaika Wasa'daika- Nimekuitikia kwa furaha yako- Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Alisema hivyo mara tatu, Akasema: "Hakuna mja yeyote atakayeshuhudia kuwa Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake kiukweli toka moyoni mwake ispokuwa atamharamisha Mwenyezi Mungu kuingia motoni" Akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu hivi nisiwaeleze watu hili ili wajipe bishara (matumaini)? Akasema: "Basi watabweteka" Akalizungumza hilo Mua'dh wakati wa kifo chake kwa kuhofia kupata dhambi.

30 - (م) عَنْ أَبِي ذَرٍّ، عَن النَّبِيِّ صلّى الله عليه وسلّم، فِيمَا رَوَى عَن اللهِ تَبَارَكَ وَتَعَالَى أَنَّهُ قَالَ: (يَا عِبَادِي! إِنِّي حَرَّمْتُ الظُّلْمَ عَلَى نَفْسِي [1] وَجَعَلْتُهُ بَيْنَكُمْ مُحَرَّماً، فَلاَ تَظَالَمُوا [2] .
يَا عِبَادِي! كُلُّكُمْ ضَالٌّ إِلاَّ مَنْ هَدَيْتُهُ؛ فَاسْتَهْدُونِي أَهْدِكُمْ.
يَا عِبَادِي! كُلُّكُمْ جَائِعٌ إِلاَّ مَنْ أَطْعَمْتُهُ؛ فَاسْتَطْعِمُونِي أُطْعِمْكُمْ.
يَا عِبَادِي! كُلُّكُمْ عَارٍ إِلاَّ مَنْ كَسَوْتُهُ؛ فَاسْتَكْسُونِي أَكْسُكُمْ.
يَا عِبَادِي! إِنَّكُمْ تُخْطِئُونَ بِاللَّيْلِ وَالنَّهَارِ، وَأَنَا أَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعاً؛ فَاسْتَغْفِرُونِي أَغْفِرْ لَكُمْ.
يَا عِبَادِي! إِنَّكُمْ لَنْ تَبْلُغُوا ضَرِّي فَتَضُرُّونِي، وَلَنْ تَبْلُغُوا نَفْعِي فَتَنْفَعُونِي.
يَا عِبَادِي! لَوْ أَنَّ أَوَّلَكُمْ وَآخِرَكُمْ وَإِنْسَكُمْ وَجِنَّكُمْ، كَانُوا عَلَى أَتْقَى قَلْبِ رَجُلٍ وَاحِدٍ مِنْكُمْ، مَا زَادَ ذَلِكَ فِي مُلْكِي شَيْئاً.
يَا عِبَادِي! لَوْ أَنَّ أَوَّلَكُمْ وَآخِرَكُمْ وَإِنْسَكُمْ وَجِنَّكُمْ، كَانُوا عَلَى أَفْجَرِ قَلْبِ رَجُلٍ وَاحِدٍ، مَا نَقَصَ ذَلِكَ مِنْ مُلْكِي شَيْئاً.يَا عِبَادِي! لَوْ أَنَّ أَوَّلَكُمْ وَآخِرَكُمْ وَإِنْسَكُمْ وَجِنَّكُمْ، قَامُوا فِي صَعِيدٍ وَاحِدٍ فَسَأَلُونِي، فَأَعْطَيْتُ كُلَّ إِنْسَانٍ مَسْأَلَتَهُ، مَا نَقَصَ ذَلِكَ مِمَّا عِنْدِي؛ إِلاَّ كَمَا يَنْقُصُ المِخْيَطُ
[3]
إِذَا أُدْخِلَ البَحْرَ.
يَا عِبَادِي! إِنَّمَا هِيَ أَعْمَالُكُمْ أُحْصِيهَا لَكُمْ، ثُمَّ أُوَفِّيكُمْ إِيَّاهَا، فَمَنْ وَجَدَ خَيْراً فَلْيَحْمَدِ اللهَ، وَمَنْ وَجَدَ غَيْرَ ذَلِكَ فَلاَ يَلُومَنَّ إِلاَّ نَفْسَهُ) .

Kutoka kwa Abuu Dhari Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- katika yale anayoyapokea kutoka kwa Mola wake: "Enyi waja wangu hakika Mimi nimeharamisha dhulma juu ya Nafsi yangu na nikaifanya kuwa ni haramu baina yenu, basi msidhulumiane, enyi waja wangu nyote ni wapotevu isipokuwa yule niliye muongoza, basi niombeni uongofu nami nitakuongozeni, enyi waja wangu nyote ni wenye njaa isipokuwa yule niliye mlisha, basi niombeni chakula nami nitakulisheni, enyi waja wangu nyote mpo uchi isipokuwa yule niliye mvisha, basi niombeni kuvishwa nami nitakuvisheni, enyi waja wangu hakika nyinyi mnakosea usiku na mchana na mimi ninasamehe madhambi yote, basi niombeni msamaha nami nitakusameheni, enyi waja wangu hamtafikia kufanya madhara mpaka mnidhuru wala hamtafanya mambo yenye manufaa mpaka mninufaishe, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wakijikusanya wote wakawa na ucha Mungu wa mtu mmoja hilo lisinge niongezea chochote katika Ufalme wangu, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wakijikusanya wote wakafanya uovu wa mtu mmoja hilo lisinge punguza chochote katika Ufalme wangu, enyi waja wangu laiti wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu binadamu na majini wangejikusanya katika uwanja mmoja wakaniomba nikampa kila mtu alicho kiomba hilo lisinge punguza chochote katika Ufalme wangu isipokuwa ni kama sindano inavyo punguza maji pindi inapo ingizwa baharini, enyi waja wangu si vinginevyo bali hakika matendo yenu yote nina wahifadhieni kisha nitawapa malipo yenu, mwenye kupata kheri amshukuru Mwenyezi Mungu, na atakayepata kinyume na hayo basi asimlamu yeyote isipokuwa nafsi yake) ((360)).