3175 - (ق) عَنِ ابْنِ مَسْعُودٍ، عَنِ النَّبِـيِّ صلّى الله عليه وسلّم قَالَ: (سَتَكُونُ أَثَرَةٌ وَأُمُورٌ تُنْكِرُونَهَا) ، قالُوا: يَا رَسُولَ اللهِ! فَمَا تَأْمُرُنَا؟ قَالَ: (تُؤدُّونَ الْحَقَّ الَّذِي عَلَيْكُمْ، وَتَسْأَلُونَ اللهَ الَّذِي لَكُمْ) .
Kutoka kwa bin Mas'udi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika ukweli ni kwamba utakuja kutokea uchoyo baada yangu na mambo msiyoyajua(uzushi)!" wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu unatuamrisha nini? Akasema: "Mtekeleze haki iliyo juu yenu, na mumuombe Mwenyezi Mungu haki yenu".
[خ3603/ م1843]